MOJA KWA MOJA: Matokeo ya uchaguzi Uganda
14:20 Tume ya uchaguzi imetoa matangazo mengine na kufikisha idadi ya vituo ambavyo matokeo yametangazwa hadi 24,342 (86.9%) kati ya 28,010. Rais Yoweri Museveni ana kura 5,288,074 (61.88%) naye Dkt Kizza Besigye kura 2,920,664 (34.18%). Tume inatarajiwa kutangaza mshindi kufikia saa kumi alasiri.
13:47 Gazeti la Daily Monitor linaripoti kuwa rais wa FDC Mugisha Muntu na Erias Lukwago wa chama cha DP wamefika nyumbani kwa Dkt Kizza Besigye eneo la Kasangati lakini wakazuiwa kuingia na maafisa wa usalama waliozingira nyumba hiyo.
13:34 Mwangalizi mkuu wa Jumuiya ya Madola Olusegun Obasanjo amekosoa baadhi ya mambo yaliyotokea wakati wa uchaguzi mkuu Uganda. Amesema haikuwa haki kumkamata na kumzuilia Dkt Kizza Besigye.
12:57 Mwangalizi mkuu wa Umoja wa Ulaya Eduard Kukan amesema hakuna ushahidi wa kuonyesha kwamba Tume ya Uchaguzi Uganda ilijifunza kutokana na yaliyotokea wakati wa uchaguzi mkuu 2011.
15:57 Mwangalizi mkuu wa Bunge la Ulaya Bw Leinen amesema kuna hatua nyingi ambazo zinafaa kuchukuliwa kuboresha uchaguzi Uganda.
12:04 Mwangalizi mkuu wa Bunge la Ulaya Jo Leinen asema kulikuwa na kasoro nyingi. Asema mfano fedha za serikali na chama lazima zitenganishwe. Asema hakukuwa na usawa katika kuwapa wagombea nafasi katika vyombo vya habari vya dola. Asema tume pia haikuwapasha raia habari vyema.
11:57 Waangalizi wa Umoja wa Ulaya: Tutatoa ripoti kamili baadaye ambayo pia itakuwa na mapendekezo ya hatua zinazofaa kuchukuliwa kuboresha mfumo wa uchaguzi Uganda.
11:56 Waangalizi wa Umoja wa Ulaya: Hatua ya kufunga usajili wa wapiga kura Mei 11 uliwafungia watu waliotimiza umri wa miaka 18 baada ya tarehe hiyo.
11:54 Hakuna mfumo wa kisheria wa kuhakikisha usawa wakati wa kampeni. Sheria za kufichua fedha za kampeni hazifuatwi na hazitekelezwi.
11:53 Waangalizi wa Umoja wa Ulaya: Visa vya kukamatwa na kuhangaishwa kwa wapinzani viliripotiwa katika zaidi ya wilaya 20. Sana waathiriwa walikuwa wa chama cha FDC.
11:52 Waangalizi wa Umoja wa Ulaya : "Tume inakosa uwazi na wadau hawana imani nayo. Tume haina uwazi katika kufanya maamuzi na katika kuwafahamisha wapiga kura kwa wakati na kwa ufasaha."
11:50 Waangalizi wa Umoja wa Ulaya washutumu kukamatwa kwa mgombea urais wa chama cha FDC Dkt Kizza Besigye jana.
11:41 Matokeo ya uchaguzi wa urais ya karibuni zaidi: Vituo 23,308 kati ya jumla ya vituo 28,010, Rais Yoweri Museveni ana kura 5,047,754 (61.55%) naye Kizza Besigye 2,826,444 (34.47%). Vituo ambavyo matokeo yametangazwa ni asilimia 83.21 ya vituo vyote

Reviews:

Post a Comment

PRINCE PRODUCT © 2014 - Designed by Templateism.com, Plugins By MyBloggerLab.com | Published By Gooyaabi Templates

Contact us

Powered by Blogger.