Madaktari Australia wapandikiza moyo
Madaktari wa Australia wamefanikiwa
Mashine iliyotumika kuuhisha moyo uliokufa na kisha kupandikiza kwa mgonjwa
 kuwarejeshea uhai wagonjwa watatu 
baada ya kupandikizwa moyo uliokufa
 katika operesheni ya kwanza kufanyika
 duniani.
Madaktari katika hospitali ya St Vincent 
mjini Sydney walitumia dawa ya kuzuia 
kuharibika iliyotengenezwa na Taasisi ya 
Utafiti wa Moyo ya Victor Chang kwa
 kupandikiza viungo kwa Michelle Gribilas,mwenye umri wa miaka 57 na Jan Damen mwenye umri wa miaka 44, huku mgonjwa wa tatu akiendelea kupona.
Moyo mmoja, ulisimama mapigo kwa dakika 20 kabla ya kuurejesha katika uhai, ukiwa umewekwa katika mashine na kuuchoma dawa ya kuzuia kuharibika.
Jan Damen na mkewe Silvana

Jan Damen, mwenye umri wa miaka 44, (akiwa katika
 picha na mke wake Silvana) alipandikizwa moyo
 uliokufa na kuupa uhai.
Wagonjwa wawili waliopandikizwa moyo (Michelle
 Gribilas, kushoto, na Bwana Damen, katikati)
 wanazungumza na daktari wa upasuaji
 Kumud Dhital
Moyo unahuishwa baada ya kupoteza uhai na
kupandikizwa. Hospitali hiyo inaamini asilimia 30 za watu watarejeshewa uhai kutokana na kugunduliwa kwa dawa hii, ambayo hupunguza kiwango cha uharibifu kwenye moyo na kuwa tayari kupandikizwa.

Moyo unahuishwa baada ya kupoteza uhai na kupandikizwa. Hospitali hiyo inaamini asilimia 30 za watu watarejeshewa uhai kutokana na kugunduliwa kwa dawa hii, ambayo hupunguza kiwango cha uharibifu kwenye moyo na kuwa tayari kupandikizwa.
Image caption Michelle Gribilas (kushoto) Jan Damen(katikati) wakizungumza na daktari wao Kumud Dhital
Michelle Gribilas (kushoto) Jan Damen(katikati) wakizungumza na daktari wao Kumud Dhita
Kabla ya operesheni hizi, madaktari wa moyo
 wamekuwa wakitumia moyo kutoka kwa watu
 waliokufa kwa asilimia 100 ambao katika uhai
 wao walitaka viungo vyao vitumiwe na watu
 wengine wenye kuhitaji, lakini sasa upatikanaji
wa moyo utaongezeka zaidi.
Dawa hiyo iliyochukua miaka 12 kuitengeneza,
 pia inasaidia kuimarisha kazi ya moyo ambao
unatolewa baada ya kifo (DCD) wakati ukianzishwa
 kufanya kazi upya.
Bi Gribilas, ambaye amestaafu na kuishi Campsie kusini magharibi mwa Sydney, amesema ni mtu tofauti kwa sasa baada ya kupandikizwa moyo mpya.



Reviews:

Post a Comment

PRINCE PRODUCT © 2014 - Designed by Templateism.com, Plugins By MyBloggerLab.com | Published By Gooyaabi Templates

Contact us

Powered by Blogger.